March 22, 2018

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 55 na 56 )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA  
ILIPOISHIA   

Nikanyanyuka huku nikiwa nimeushika mkono wa mama Mariam, nikasogea taratibu hadi sehemu alipo simama mama Mariam, neneja huyo akanitazama kwa macho ya dharau huku akinipandisha na kunishusha na macho yake.
“Na wewe dada mzima unamtongoza jimama kama hili, unataka mukasaganeee eheee?”
Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama meneja huyu.
“Nakuuliza usinikodolee macho kama umechomekwa mbo** ya mkund………”
Sikumruhusu kumalizia sentensi yake, nikamtandika ngumi ya pua, iliyo muangusha chini mzima mzima na kutoa kishindo kizito hadi wapishi wwalipo jikoni wakatoa kushangaa ni kitu gani kinacho endelea huku nje.
   
ENDELEA
“Uwe na adamu na wanawake unao waona, pumbavu wewe”
Nilizungumza kwa sauti ya kike ila yenye kijiujazo kwa mbali hadi mama Mariam akanitazama usoni mwangu. Meneja huyo akajizoa zoa na kunanyuka huku akijifuta futa vumbi kililo jaa kwenye suti yake, hakuna mtu aliye msemesha zaidi ya kubaki kumuangalia, taratibu akaondoka akiwa apole kama sio yeye aliye kuja akitukana matusi mfululizo kwetu.
“Asante sana binti ila mimi kwangu kibarua ndio kimekwenda na maji”
“Usjali, hakuna jambo kama hilo”
“Mmmm”
“Yaa niamini mimi”
Nikjitahi kuzungumza kwa sauti ya kike ili mama Mariam asinifahamu kabisa kwa maana kunifahamu kwake inaweza ikawa ni tatizo jingine kwa maana bado siweza kumuamini mara moja isitoshe nipo kwenye tatizo kubwa kama hili la kutafutwa nchi nzima kama gaidi.
 
“Naomba unitengenezee juisi na uniletee katika chumba changu”
“Juisi gani?”
“Juisi ya parachichini lililo changanywa na pensheni.”
Nikamtajia namba ya chumba mama Marimu kisha nikampa shiling elfu hamsini.
“Ya nini hii?”
“Kwa ajili ya usumbufu wa kuniletea juisi hiyo chumbani kwangu, nahitaji jagi zima”
“Sawa binti”
Nikaondokea huku nikitamani kuangalia nyuma kumuangalia mama Mariam ila nikashindwa, nikapanda gorofani kwa kutumia lfti, nilipo fika katika mlango wa chumba changu nikabisha hodi, Monica akanifungulia mlango na nikaingia ndani.
“Mbona umechelewa honey?”
“Nilikuwa natoa maelekezo kwa wapishi”
“Ahaa sawa”
 
Nikapanda kitandani huku nikiwa nimeshika rimoti ya Tv, niliyo ichukua mkononi mwa Monica, nikaanza kubadilisha chaneli moja baada ya nyingine, kuangalia ni kitu gani ambacho kinaendelea. Hapakuwa na jambo jipya zaidi ya picha yangu kutangazwa. Mlio wa simu ya Monica ndio ulio nifanya niweze kumgeukia na kumtazama, akanitazama machoni kisha akaipokesa simu yake.
“Halooo”
“Nini?”
“Ohooo Mungu wangu, jamanii”
“Ok ok”
Monica alizungumza huku akiwa amebadilika na kuchanganykiwa, wala sikufahamu ni jambo gani ambalo linamsumbua. Akakata simu na kuiweka pembeni na kuanza kumwagika na machozi, ikanibidi kumvuta karibu yangu na kumkumbatia
“Honey kuna kitu gani kilicho tokea”
“Ni mdogo wangu ohoooo Mungu wanguu jamani weeee”
“Mdogo wako amepatwa na nini?”
 
“Amegongwa na gari ohooo Mungu wangu”
Nilihisi na mimi kama mwili wangu ukizizima, nikawa kama nimepigwa na bumbuazi na wala sikuhitaji kusikia ni kitu gani ambacho atakizungumza kitakacho muhusu mdogo wake, nikaichukua simu yake na kushuka kitandani na kusimama mbele yake huku nikimtazama Monica aliye jiinaminia na nywele zake kuzichangua akionyesha ni kwa namna gani alivyo patwa na uchungu wa tukio lililopo mbele yetu. Nikaipiga namba hiyo, baada ya muda mfupi ikapokelewa.
“Habari”
Nlizungumza kwa sauti ya kike
“Salama tu dada”
“Kuna kitu gani kinacho endelea, kwa maani nipo na Monica baada ya kumaliza kupokea simu yako amechanganyikiwa kabisa?”
“Ohoo ni kweli dada yangu, hapa nimempa taarifa mdogo wake amegongwa na gari, na hapa hali yake ni mbaya sana na amewahishwa katika hospitali ya Bombo”
“Ok ngoja nifanye utaratibu, ila kuna kitu chochote kingine kinacho hitajika kama pesa au laaa?”
 
“Hapana hapa majirani zao ndio tupo hospitalini tunaangalia ni kitu gani ambacho kinaweza kuendelea”
“Ok asante”
Nikakata simu na kupiga magoti chini mbele ya Monica na kukinyanyua kichwa chake na kumtazama usoni.
“Baby baby, nisikilize”
Monica akabaki amenikodolea macho huku ananitazama usoni asinijibu kitu cha aina yoyote.
“Mdogo wako hajafariki, na hali yake madaktari wanaendelea kuishuhulikia, nakuomba utulie, tumuombe Mungu aweze kutusaidia madaktari waweze kufanikiwa kwa kile wanacho kihangaikia mbele ya mdogo wetu”
“Dany nahitaji kwenda Tanga, sasa hivi”
Nikajikuta nikishusha pumzi, nikamtazama Monica usoni kwa dakika moja pasipo kumsemesha kitu cha aina yoyote.
 
“Yaaa nahitaji kwenda Tanga. Dany natambua unanipenda na mimi nakupenda na nilikuahidi kwamba nitakuwa pamoja na wewe kila sehemu ila kwa hili la mdogo wangu, please Dany nakuomba niende. Nakuhakikishia kwamba nitalinda penzi langu hadi pale tutakapo onana”
Nikajikuta nikimkumbatia Monica kwa nguvu, huku machozi yakinilenga lenga.
“Dany kamilisha kile ulicho kianza, usikate tamaa, hata kama iweje nitahakikisha unaibuka na kuwa shujaa katika hili”
Monica alizidi kuzungumza huku machozi yakimwagika mfululizo usoni mwake.
“Nakuruhusu, ila sinto hitaji usafiri na basi”
“Noo Dany sihitaji uniepeleke Tanga kwa gari nitapanda basi tu”
“Hapana, vaa tunaelekea uwanja wa ndege sawa”
“Sawa”
 
Monica akavua taulo aliko kuwa emajifunga kiunoni mwake, na kuanza kuvaa suruali ya jease kwa haraka haraka kisha akavaa na tisheti, nywele zake akazibana vizuri kidogo.
“Nitakuongezea na pesa ili matibabu ya mdogo wako yawe mazuri, ikishindikana mlete huku Dar es Salaam”
Nilizungumza huku nikiwa nimeshika Monica kiuno chake, akimalizia kuchana nywele zake vizuri. Baada ya kuhakikisha kila kitu kipo sawa, tukatoka na kufunga mlango ila baadhi ya vitu nikaviacha kwenye hiki chumba. Tukashuka chini, Monica akiwa amebeba brufcase yenye pesa. Tukaingia kwenye gari na kueleka uwanja wa ndege wa mwalimu Julius Nyerere. Foleni haikuwa ndefu sana, tukafanikiwa kufika salama sakamin.
 
Tukashuka kwa pamoja tukaelekea kwenye sehemu ya kukata tiketi kwa ndege za kueelekea mikoani, kwa bahati nzuri kuna ndege inaondoka muda mchache kuelea Tanga na ni siti moja tundio ilikuwa imebakia. Tukakumbatiana na Monica.
“Dany wangu nakuomba uweze kubaki salama”
“Asante unijulishe kila kitu kinacho endelea na uwe makini sana”
“Sawa”
Monica akashindwa kunipiga mabusu kutokana na muonekano wangu na laiti akifanya hivi itakuwa ni habari ya kurushwa kwenye mitandao ya kijamii. Akaeelekea katika sehemu ambayo abiria wa kuondoka wanatakiwa kwenda. Nikaondoka uwanja wa ndege na kurudi hotelini huku kichwa kikiwa na mawazo ya kujiuliza ni wapi nianzie katika kuifanya kazi yangu.
 
“Samahani dada nina ujumbe wako wapa kutoka kwa watu wa jikoni”
Muhudumu alizungumza huku akinitazama usoni mwangu
“Ndio”
“Waliniambia ukuridi niwafahamishe waweze kukuleta chakula chaho ulicho agiza”
“Sawa walete tu”
Nikaondoka na kueleka chumbani kwangu, nikaufunga mlango kwa ndani na kujitupa kitandani. Nikataka kuvua umbo la plastiki nililo livaa, ila nikakumbuka kwamba kuna wahudumu wa jikoni watakuja humu ndani.  Ikanibidi kubaki katika muonekano wangu huu huu. Nikashuka kitandani na kuchukua laptop yangu nikaifungua, moja kwa moja nikaifungua video aliyo nitumia mama kwa umakini, nikachukua simu na kumpigia mama.
 
“Eheee”
“Mama umeweza kufanikiwa na kutambua kwamba hili jengo lipo sehemu gani?”
“Jengo gani?”
“Kwenye hii video ambayo umenitumia”
“Sijaweza kufahamu hadi sasa hivi ila bado ninaendelea kutafuta kuweza kufahamu ni eneo gani”
“Sawa mama kwa maana nahitaji kumshusha K2 kutoka juu alipo hadi chini”
“Kumshusha kivipi?”
“Kumfilisi kama walivyo kufilisi wewe”
“Sawa mwanangu kama nilivyo kuambia ufanye, rudi na kichwa chake hapa”
“Sawa mama baadae”
 
“Haya”
Nikakata simu huku, hata kabla sijafanya chochote mlango ukagongwa, nikanyanyuka kwenye sofa, nikapiga hatua hadi mlangoni na kufungua mlango. Nikakutana na muhudu wa chakula, akanikabidhi chakula changu, sikuwa na hamu hata ya kukila chakula hichi. Haukupita muda mwingi mlango ukagongwa, nikanyanyuka na kwenda tena kufungua mlango, nikakutana na mama Marima akiwa ameshika jagi la juisi.
“Karibu ndani”
Nilizungumza kwa sauti ya upole ya kike huku nikimtazama mama Mariam aliye nitazama machoni kwa upele kisha akainga na jagi lake akiwa amelishika, nikafungu mlango kwa funguo na kumkaribisha aweze kukaa kwenye sofa, japo usoni wasiwasi mwingi umemtawala.
“Ahaa nimekuletea, ninaomba niende kwa maana hadi sasa hivi sijafahamu hatima ya kazi yangu”
“Ohoo sawa mama yangu, hakuna shida ila ninahitaji kufahamu baadhi ya vitu vichache kutoka kwako”
“Nakusikiliza mwanangu”
 
“Kwani hii kazi unalipwa kiasi gani kwa maana sioni sababu ya wewe kuendelea kufanya kaz hapa”
“Hapa ninalipwa laki mbili tu”
“Mshahara mdogo sana huo”
“Ahaa binti yangu, ukisema hapa mjini uweze kuacha kazi ni ngumu kupata kazi”
“Ni kweli, vipi una mtoto?”
“Nilikuwa naye mmoja wa kike”
“Amekwenda wapi?”
“Ni miaka miwili sasa mepita, alipotea katika mazingira ya kutatanisha, nikatoa taarifa polisi juu ya swala hilo ila polisi hawakunisaidia kwa chochote. Tangu mwanangu kuondoka nimekuwa ni mtu wa mateso”
Mama Mariam alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, taarifa aliyo niambia, ikaanza kuniumiza kichwa changu kufikirini imekuwaje kuwaje hadi Marim akapotea katika mazingira ya kutatanisha.
“Watu wanavyodai kwamba Maram alitwekwa na watu wasio julikana na hao ndio walio weza kuondoka naye hadi muda huu”
 
“Una uhakika kwamba alitekwa?”
“Sina uhakika katika hilo, ila……….”
Mama Marim akaka kimya akanitazama usoni mwangu, kisha akanisogelea huku akinikazia macho yake. Akauchukau mkono wangu wa kushoto na kuutazama kiganja chake. Akataka kuzungumza kitu ila akaendelea kunitazama hadi nikaanza kuogopa. Akashusha pumzi nyingi huku akikiachia kiganja changu. Akasimama na kuanza kupiga hatua za haraka huku akikimbilia mlangoni, nikasimama na mimi kwa haraka na kumuwahi kumzuia mlamgoni.
Nikatazama jinsi kifua cha mama Marim jinsi kinavyo nyayuka kwa mapigo ya moyo yanavyo mwenda kasi sana.
“Naomba utulie mama yangu uniembie ni nini kilicho tokea”
Mama Marim akaendelea kunikazia macho huku machozi yakimwagika uson mwake mfululizo. Akayafumba macho yake kwa muda nikabaki nikiwa ninamtazama, gafla nikastukia akilivuta wigi langu la kichwani na nikabaki na upara wangu, jambo lililo nifanya mapigo ya moyo yaniende kasi sana kwani mama Mariam ndio mtu wa kwanza kuweza kunifahamu uhalisa wangu.
“DANYYYYYYYY”   
Marim aliniita kwa mshangao huku akiwa amenikazia macho tofauti na hata mara ya kwanza.

                            AISIIIII……….U KILL ME 56

Ukimya wa takribani dakika moja ukapita, sote tukiwa kimya pasipo kuzungumza kitu chochote wala kupiga hatua ya kwenda popote. Nikastukia kofi zito likitua shavuni mwangu, kisha mama Marim akanikumbatia kwa nguvu na kuanza kumwagikwa na machozi mfululizo.
Taratibu machozi yakaanza kunimwagika na mimi, mama Marima akaniachia na mikono yake akanishika mashavuni kwa viganja vyake vilaini kisha akanipiga busu la mdomo, lililo pelekeea kujikuta tuazama kwenye denda zito.
Taratibu tukaanza kurudi nyuma huku tukiendelea kunyonyana denda, mama Mariam akaanza kuvua nguo moja baada ya nyingine. Nikalivua gauni langu na kubakiwa na umbo la plastiki lililo mfanya mama Marima kucheka.
“Ndio nini Dany?”
“Nifungue”
Mama Marim akanifungua zipu ya umbo hili la plastiki, nikalivua, nikamsukuma mama Marim kitandani, uzuri wa mama Mariam bado upo vile vile, japo yupo katka kipindi kigumu cha kupotelewa na binti yake ila kusema kweli bado anajua kujitunza.
 
Mama Marim akanivua boksa yangu na kuanza kumnyonya jogoo wangu kwa fujo, alipo ridhika akahamia kifuani kwangu na kuanza kunyonya kila sehemu ya kifua changu, mikono yangu sikutaka kuiacha ikae kiholela holela, na mimi nikawa na kazi ya kucheza na maziwa yake, kila jinsi ya kuyaminya ninavyo yaminya ndivyo ninavyo nilivyo fanya.
Nikaanza kucheza na kitumbua cha mama Marima, nilipo hakikisha kimelainika vya kutosha, akapiga magoti kitandani huku kifuani mwake akiwa ameulalia mtu. Taratibu jogoo wangu akazama kwenye kitumbua chake, na kumfanya atoe mguno ambao kwa kipindi kirefu sikuweza kuusikia. Mama Marima, akaanza fujo za kukata kiuno chake kiasi kwamba akanifanya na mimi nizidi kuongeza kasi ya kuhakikisha kwmaba ninaendana na kasi ya kiuno chake na makalio yake yanayo cheza cheza kwa kutingisha.
 
    Shuka mito mingine iliuyo salia, vikajikuta vikianguka chini, kwa kurupushani tunazo zifanya, inaonyesha ni kwa kiasi gani tulivyo weza kuwa na hamu kali japo mimi nimetoka kulala Monica, ila kwa mama Mariam sikuonyesha udhaifu wowote wa kwamba nimetoka kungonoka muda ulio pita. Mama Maria, akaweza kuhimili mchezo mzima hadi ninafika mwisho kabisa, yeye akawa amesha jifunga magoli zaidi ya sita niliyo weza kuyashuhudia kwa kumwaga maji yaliyo lainisha uwanja.
“Dany kumama….o siku zote ulikuwa wapi mseng** wewe?”
Mama Marim alizungumza huku akihema kwa nguvu, jasho likimwagika shingoni
“Ni stori ndefu ila na wewe bado mbichi kama sio mtu mzima”
“Ahaaa niliitunza hii kum*** tangu ile siku unitomb** sijakutana na mwanaume na nilisha kataga tama kwamba siwezi kukuona, husuani pale nilipo ona unatafutwa kama gaidi ndio nikaishwa nguvu kabisa, kuna lizee likawa linananitaka laity ingekuwa si kuonana leo, kesho ningemkubalia”
 
“Duuu, hivi imekuwaje ukaweza kunifahamu mimi?”
“Nilikutilia mashaka tangu pale ulipo kuwa unaiambia kuhusiana na juisi, ila sikuwa na mashaka sana kutokana siku hizi wanawake wapo wanao fanana na wanaume, ila nilipo kaa pale kwenye kochi, nikaweza kukufahamu kwamba ni wewe japo ulikuwa unajifanya kuzungumza kwa sauti ya kike”
“Hahaaaa”
“Dany yaani mimi hata ungejibadilisha vipi ningekufahamu, lipsi zako siwezi kuzisahau, kuzungumza kwako ndio kabisa, kulinifanya niweze kukufahamu.”
“Chumba changu kwako bado kipo?”
“Kipo japo kuna wapelelezi walikujaga kipindi fulani cha nyuma, wakawa wanakigagua sijui walipata nini wakaondoka zoa”
“Kipindi wanakuja Marima alikuwa amesha potea?”
“Ndio, nikawaelezea juu ya jambo hilo ila hakuna aliye weza kunisaidia”
 
“Na nyumbani kwako kuna wapangaji wengine?”
“Wapo tena vyumba vyote vimejaa”
“Leo tutakwenda kwako”
“Kwangu na kutafutwa kwako si watakuja kunikamata hadi mimi?”
“Hapana nahitaji kuhakikisha kwamba tunampata Marim kwanza”
Mama Marim akaka kimya huku akinitazama usoni mwangu kisha akatingisha kichwa na kukubaliana na ombi langu japo usoni mwake ninamuona ana mashaka mengi.
“Naomba unisaidie kukusanya hizi guo uniwekee kwenye begi”
“Sawa”
Nikashuka kitandani na kuelekea bafuni, nikaoga huku nikiwa makini sana kwa masikio yangu kuweza kuyatega kuhakikisha kwamba mama Marima apigi simu kwa mtu wa aina yoyote. Nikatoka bafuni na kumkuta mama Mariam akiwa anamaliza kufunga zipu ya begi. 
 
“Kuna tisheti nyeusi ilikuwa hapa kwenye sofa ipo wapi?”
“Nimeiweka kwenye begi”
“Nitolee pamoja na gauni niliko kuwa nimelivaa”
“Sawa”
Mama Marima akanitolea kile nilicho kihitaji, kisha akaingia bafuni kwa ajili ya kuoga, nikaanza kuvaa tisheti kisha boksa, nikavaa umbo la plastiki. Nilipo hakikisha lipo vizuri nikavaa na gauni nililo kuwa nimelivaa, nikajiweka sawa. Nikachukua bastola zangu na kuziweka kwenye kipochi changu cha mkononi. Mama Marim akatoka bafuni akavaa nguo zake, tulipo hakikisha kwamba tupo zivuziri, mama Marim akatangulio kutoka chumbani humu, kisha baada ya dakika tano na mimi nikatoka nikiwa nimebeba kipochi pamoja na begi la nguo, kwa muonekano huu wa kike hakuna mtu anaye weza kunigundu kwa haraka.
 
    Nikaeleka lilipo gari langu, nikaingiza begi la nguo kwenye buti, begi la pesa zangu nikalifungua kuhakiksha kama pesa yangu ipo, nikakuta ipo sawa sawa. Nikaingia kwenye gari kama nilivyo kubaliana na mama Marima kwamba nitamkuta kwenye kituao cha daladala, mbele kidogo kutoka katika hoteli hii ndivyo alivyo fanya. Nikafika katika kituo hicho na kumkuta mama Mariam akiwa amesimama, nikashusha kioo huku nikipigia honi, kwa maana halifahamu gari langu. Alipo niona kwa haraka akapiga hatua na kuzunguka upande wa pili wa gari, akaingia na tukaondoka eneo hili.
“Ila Dany mwenzako nina wasiwasi kama nini?”
“Wasiwasi wa mimi kukamatwa?”
“Ndio”
“Niamini mimi, nitakaa hivi mpaka kazi yangu nitahakikisha kwamba nmeimaliza”
 
“Mmmm”
“Yaa niamini, nitakulinda na nitahakikisha Marim ninampata”
“Sawa”
Foleni ya ndio ikatufanya kuchelewa kufika Sinza. Nikasimamisha gari nje ya geti la mama Marima, kisha akashuka, hapakuwa na mabadiliko mengi kwenye huu mtaa zaidi ya baadhi ya nyumba kupwakwa rangi. Nilipo jiridhisha usalama wa mtaa huu upo nikashuka kwenye gari huku nikiwa nimebeba kipochi changu mkono wa kushoto na funguo ya gari nikiwa nimeishika mkono wa kulia. Mama Maria makatangulia mbele, tukakuta wadada wawili wakiwa wamekaa kwenye kibaraza wakisukana, wakamsalimia mama Marima kisha wakanisalimia na mimi, kama kawaidia nikawajibu kwa sauti ya kike kisha tukaingia ndani. Nilipo ona pazia la mlangoni mwangu mwili wangu ukasisimka na kukumbuka matukio mengi yaliyo weza kutokea katika chumba hichi. Mama Marim akanikaribisha chumbani kwake.
“Chumba chako kumbe kizuri hivi?”
 
“Yaaa namshukuru Mungu amenisaidia saidia kuongeza baadhi ya vitu”
“Ahaaa sawa sawa”
“Unakunywa nini?”
“Mmmm hapana ila sijui naweza kwenda kwenye kile chumba changu?”
“Hapana Dany”
Mama Mariam alizungumza kwa sauti ya upole huku akinisogelea karibu yangu
“Kile chumba hadi sasa hivi nahisi kuna mpelezi humu ndani”
“Ni nani huyo?”
“Hao wadada wawili walio kaa hapo nje, siwaamini kabisa kwa maana sifahamu hata kazi wanayo ifanya, wanatoka usiku wanarudi asubuhi sasa sifahamu wanafanya kazi gani”
“Ahaaa basi usijali leo nitaanza kuwafwatilia”
 
“Dany ndio utazidi kujiongezee matatizo”
“Usijali katika hilo”
Siku nzima nikashinda chumbani kwa mama Marim, akapika chakula cha mchana tukala kisha tukaendelea kutazama filamu kwenye Tv iliyopo humu chumbani mwake.
“Ikifka usiku naomba nikachukue nguo kwenye chumba changu”
“Sawa ila uwe makini”
“Sawa”
Masaa yakazidi kukatika na kuzidi kusonga mbele, ilipo timu saa nne usiku, kila watu wakiwa katka vyumba vyao, nikaeleka kwenye chumba changu ambapo mama Marim alinikabidhi funguo ambayo kama mama mwenye nyumba huwa hubaki nayo na mpangaji humpatia mbili. Nikaingia chumbani kwangu, sikuwasha taa yoyote, vitu vyangu kwenye chumba nikavikuta japo vimechanguliwa changulia, ikionyesha watu walio kuja kufanya upepelezi wao walipo maliza hawakukipanga chumba changu. 
 
Nikafungu kabati la nguo, nikachukua suruali yangu nyeusi, pamoja na koti moja aina ya lazier. Nikachukua na kofia ya kot hili, kisha nikachukua na raba nyeusi. Kwa tahadhari kubwa nikatoka chumbani kwangu na kukifunga chumba.
Nikaingia chumbani kwa mama Marima, nikavua nguo zangu za kike, kisha nikavaa nguo zangu za kiumetayari kwa kuhakikisha kwamba ninaianza kazi yangu iliyo nileta Dar es Salaam. Nilipo maliza kuvaa nguo na viatu, nikaivaa kofia yangu na kusimama mbele ya kioo cha kabati lililopo humu chumbani kwa mama Marim.
“Dany Dany wale wasichana ndio wanatoka”
Mama Marim alizungumza kwa sauti ya chini huku akiwa amefungua pazia la dirisha linalo elekea getini, nikawahi kuchungulia, nikawaona mmoja wao akiwa amemalia kufunga getii. Nikatao bastola zangu kwenye pochi na kuchomeka moja nyuma ya kiuno changu na nyengine nikaichomeka kwenye soksi za mguu wa kushoto.
 
“Natoka by saa kumi nitakuwa hapa”
“Sawa kuwa makini”
“Sawa naiomba hiyo simu yangu hyo hapo mezani”
Mama Marim akaniletea simu yangu na kunikabidhi. Nikaiweka ufukoni huku nikiwa nimeiweka mlio wa mtetemesho(Vibration).
Nikatoka ndani kwenye kordo hapakuwa na mtu moja, kwa moja nikatoka nje kabisa, nikafungua geti nikachungulia kwa nje, nikawaona wale mabint wakimalizia kukatiza mtaa na kueleka mtaa mwengine. Nikaanza kutembea kwa mwendo wa haraka hadi kwenye kona waliyo kata, nikawaona wakipanda pikipiki moja. Na mimi nikasimamisha pikipiki, nikapanda
 
“Ifwate ile pikipiki ya boksa iliyo ondoka eneo hili”
“Poa bosi”
Kutokana na uvaaji wangu na kofia niliyo ivaa ni vigumu sana kwa dereva huyu kuweza kunifahamu kama mimi ni gaidi. Tukaendelea kuwafwatilia wasichana hawa ambao hadi sasa wanaeleka maeneo ya Tegeta.
“Kaka huku ni mbali na huu ni usiku”
Dereva wangu alianza kulalamika
“Wewe twende, shida yako si pesa”
“Japo pesa ninaipenda, ila naangalia pia usalama wangu”
Dereva alizungumza huku akipungumza mwendo wa pikipiki na kusimama kabisa. Nikachomoa bastola yangu ya kiunoni mwangu na kumuelekezea. Kwa ishara nikamuomba aweze kushuka, kwa maana yeye ndio amenilazimisha mimi kumshusha kwa kutuma nguvu. Kutokana anapenda usalama wake na maisha yake akashukataratibu kwenye pikipiki. 
 
“Kimbia”
Dereva huyo akaanza kujikwaa kwaa huku akikimba. Nikapanda pikipiki yake hii aina ya boxer na kuanza kuifwatilia pikipiki waliyo panda wasichana wanao ishi nyumbani kwa mama Mama Caro.  Wakakatiaza kwenye moja ya njia inayo elekea kushoto mwa barabara na kuendelea na safari na huko wanapo elekea kuna majumba makubwa ya kifahari. Na mimi kwa umbali ambao hawawezi kustuka kwamba nina wafwatilia, nikakunja. Kwa mbali nikawaona wasichana hao wakishushwa kwenye moja ya jumba la gorofa tatu ikanibidi kusimamisha pikipiki yangu.
Wakazungumza na dereva huyo kwa sekunde kadhaa kisha wakaingia ndani na dereva huyo akageuza na kuondoka, nikaendesha pikipiki yangu hadi karibu na jumba hilo, nikaisimamisha pembeni kwenye moja ya mti wenye giza totoro kisha nikaanza kutembea kwa mwnedo wa haraka hadi kwenye jumba hili.
 
Nikakumbuka tukio la siku nilipo upanda ukuta wa jumba lililo kuwa lina wahifadhi wapiganaji wa kikundi cha kigaidi cha Al-SHABAB. Japo kwa juu ukuta huu umepitishiwa nyaya za umeme sikulijali hilo, nikarudi hatua kumi nyuma, nikakimbia kwa kasi na kuuparamia ukuta huo kwa kasi nikajivuta juu, kwa umakini mkubwa pasipo kugusa nyaya hizi za umeme nikajivuta juu kuchungulia ndani. 
 
Nikaona gari tatu za ikulu ambazo anatembelea raisi zikiwa zimesimamishwa kwenye maegesho huku walinzi walio valia suti nyeusi wakiranda randa kika eneo.  Nikamuona Babyanka akitoka kwenye mlango wa jumba hili la kifahari, akamuita mmoja wa walinzi na kuzungumza naye kisha akageuza kuchwa chake na kutazama sehemu nilipo na macho yetu yakakutana jambo lililo mfanya Babyanka kuchomoa bastola yake na kuanza kufyatua risasi kadhaa kueleka sehemu nilipo.
                                                                                  ITAENDELEA

No comments:

Post a Comment