NIMEMSIKILIZA kwa makini, Dk. Willibroad Slaa, aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema na mgombea urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu. Anaandika Saed Kubenea… (endelea).
Akihojiwa na kituo cha televisheni cha Star TV, Dk. Slaa alimtuhumu Edward Lowassa kuwa ni fisadi na akataka wananchi kumchagua “mgombea mwenye nafuu ya ufisadi.” Akamtaja John Pombe Magufuli.
Ameeleza pia kuwa taarifa mpya aliyonayo na ambayo aliitumia katika mkutano wake na waandishi wa habari Jumanne iliyopita, kuhusu sakata la Richmond, aliipata kutoka kwa Dk. Harrison Mwakyembe, aliyekuwa mwenyekiti wa kamati Teule ya Bunge, juu ya Richmond.
Niliamua kutojibizana na Dk. Slaa – rafiki yangu wa miaka mingi – katika mradi wake huu. Lakini kwa hapa alipofika, uvumivu umenishinda. Sitaruhusu mtu mzima, anayejiita padri na ambaye alitaka kuwa rais wetu, kuendelea kulindanganya taifa na kuwapotosha wananchi.
Hivyo basi, nimeamua kuanzia leo hii, kukabiliana na Dk. Slaa kwa kila kona ili ukweli ufahamike. Kwa kuanzia, leo hii – Jumamosi, naelekea mkoani Mbeya ambako nitahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara katika jimbo la Kyera, linaloshikiliwa na Mwakyembe, swahiba mpya wa Dk. Slaa.
Nikiwa Mbeya nitaeleza ukweli wa kilichotokea na kile ambacho Dk. Slaa anakificha.
Aidha, nikirejea Dar es Salaam, nimepanga kuitisha mkutano na waandishi wa habari, kueleza ukweli uliokamilika kuhusu Dk. Slaa na mkewe Josephine Mushumbuzi na sababu ya yeye kususia chama.
September 7, 2015
Home
/
NEWS
/
UDAKU
/
KIMENUKA MBAYA! Baada ya DK SLAA Kumwaga Mboga, sasa KUBENEA Amwaga UGALI Kwa Style Hii!
KIMENUKA MBAYA! Baada ya DK SLAA Kumwaga Mboga, sasa KUBENEA Amwaga UGALI Kwa Style Hii!
About Unknown
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Related Posts:
UDAKU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment