Headlines zimeendelea kwenye mwaka huu wa Uchaguzi 2015 ambapo UKAWA sio
jina geni kwa Watanzania, vyama mbalimbali vya upinzani vikiwemo
CHADEMA na C.U.F vilijiunga na vinataka kumtangaza mgombea mmoja
atakaewawakilisha.
Zitto Kabwe ambaye aliondolewa kwenye chama cha CHADEMA, alijiunga na
chama cha A.C.T Wazalendo March 2015 ambapo siku kadhaa baadae chama
hicho kilitaka kujiunga na UMOJA WA KATIBA YA WANANCHI (UKAWA) lakini
imeshindikana, haya hapa chini ndio maneno ya Zitto Kabwe July 26 2015.
‘Leo siku nzima nilikua nina kikao cha mashauriano na viongozi wa chama
wa kata zote za mkoa wa Dar es salaam ( mikutano mikuu ya majimbo 10 ya
Dar) jumla ya wajumbe 1023 walihudhuriam, tumesisitiza kuwa hatutajiunga
UKAWA… ikumbukwe kuwa tuliomba utaratibu wa kujiunga UKAWA mwezi Aprili
mwaka 2015 na hatujajibiwa rasmi lakini moja ya chama ndani ya UKAWA
kilitangaza kuwa hawatutaki‘ – Zitto Kabwe
‘Hata juzi kwenye gazeti la Mawio waliandika kuwa tumefukuzwa UKAWA,
sisi tumeamua kuingia kwenye uchaguzi wenyewe.. tarehe 10 Agosti 2015
tutatangaza mgombea Urais tutakayemuunga mkono baada ya mkutano mkuu wa
kidemokrasia wa ACT Wazalendo.
Tutanadi #AzimioLaTabora kama zana ya kuleta mapinduzi katika nchi yetu‘- Zitto
Kwenye sentensi nyingine ya Facebook aliyoandika Zitto Kabwe saa kadhaa kabla ya hiyo ya juu aliandika:
'ACTWazalendo Tutaingia kwenye uchaguzi wenyewe. We will go it alone
as a party to defend our principles. Mkutano Mkuu wa Chama wa
Kidemokrasia ( National Convention) utafanyika tarehe 10 Agosti 2015′
No comments:
Post a Comment