March 24, 2016

Obama acheza densi ya tango Argentina


Rais Obama alisisimua watu waliohudhuria dhifa ya jioni katika ikulu ya rais mjini Buenos Aires, Argentina baada ya kucheza densi maarufu ya tango na mnenguaji wa kike. Mkewe Michelle naye alicheza na mtumbuizaji wa kiume.
Dhifa hiyo iliandaliwa na mwenyeji wake Rais Mauricio Macri Jumatano.
Baada ya kumaliza, waliohudhuria waliwashangilia.

No comments:

Post a Comment