September 10, 2015

Kutoka Kigoma: elimu ya uzazi wa mpango yaendelea kutolewa

Wadau,

Elimu ya uzazi wa mpango bado haijamfikia kila mtu, kuna jitihada za makusudi zinazofanyika na watu binafsi, mashirika pamoja na serikali ili kuendelea kueneza elimu hii.

WLF kupitia kampeni ya Thamini Uhai nayo haipo nyuma, wahamasishaji jamii kutoka Kigoma wanatuhabarisha jinsi harakati za kufikisha ujumbe kwa umma zinavyoendelea.

Mhamasishaji jamii, Upendo Reuben, ametuma picha hii ya wanafunzi wa Sekondari ya Katabuka, manispaa ya Kigoma wakisikiliza elimu ya uzazi wa mpango. 

Click image for larger version. 

Name: wanafunzi wa sekondari ya katabuka.jpg 
Views: 35 
Size: 92.5 KB 
ID: 285317

Mfanyakazi wa afya, Jockdan, anatuhabarisha kuhusu elimu ya uzazi wa mpango unaofanywa kituo cha afya Kimwanya kwa njia ya picha.

Click image for larger version. 

Name: kutoka kigoma.jpg 
Views: 27 
Size: 63.2 KB 
ID: 285321


Mhamasishaji jamii kutoka Wilaya ya Kibondo, mkoani Kigoma, Benjamin, ametuma picha hii ya familia yenye watoto wengi wanaotunzwa na Bibi (wa pili kushoto). Bibi ameomba watoa huduma waongeze bidii kutoa elimu ya uzazi wa mpango.


Click image for larger version. 

Name: bibi na wanawe.jpg 
Views: 35 
Size: 111.1 KB 
ID: 285322


Hayo yanatoka Kigoma, upande wako mambo yakoje? Elimu ya Uzazi wa Mpango inapenya vilivyo au inachelewa?

Karibu.

No comments:

Post a Comment