October 30, 2014

LULU ANGEKUWA HOLYWOOD INGEKUWA HIVI DUH HUYU NDIO LULU....MICHAEL


Star mkubwa wa filamu nchini Tanzania Lulu Elizabeth Michael anaonekana kumpenda sana Justin Bieber kama alivyowahi kueleza huko nyuma kuwa anampenda kweli kiasi cha kumfuatilia kwa ukaribu Selena Gomez ambaye ni girfriend wa Bieber.

  
 Hata hivyo Lulu ameonekana kuachia ngazi kwa Bieber baada ya takribani miaka 4 akiwa anaugulia penzi lake moyoni bila mafanikio !
 
Kama unavyojua vituko vya Lulu haviishi, kupitia Instagram Lulu aliweka picha ya Selena na kumsifia kuwa yupo vizuri hasa kwa uzuri na kuvaa zaidi yake huku akimwita mke mwenzake.
 
Hata hivyo mashabiki walimwambia Lulu kuwa Selena ni mzuri ndiyo ila hamfikii Lulu kwa uzuri na hata kuvaa ingawa Lulu bado yupo Bongo kwani angekuwa huko mtoni angekuwa tishio kwa Selena zaidi ya mara mbili.
 
"Mke mwenzangu yuko vizuriiii mnooooooo.....Kwa kupendeza huku Nimeamua kuachia ngazi rasmi iii ii. ....He is all yourssssss...!!!#WCW" aliandika Lulu na kuweka picha ya Selena akiwa amevaa kigauni cha rangi nyekeundu.
 
Ukweli ni kuwa Selena Gomez ni maarufu zaidi ya Lulu kwasababu anajulikana dunia nzima kutokana na nature ya entertainment industry ya Marekani lakini kwa suala la uzuri na mvuto bado Selena na Lulu wanatoana jasho kwa ukaribu sana na pengine Lulu kumzidi Selena.

 Selena ana utajiri mkubwa kuliko Lulu lakini kwa ambao wameona filamu za Selena ni kuwa kwa kipaji cha acting Lulu ana kipaji kuliko Selena sema kibongobongo ndo hivyo bado kipaji kinashindwa kutambulika dunia nzima kutokana na sababu mbalimbali ikwemo waongozaji duni wa filamu.
  
 Ila Lulu angekuwa Hollywood pamoja na Selena na Justin Bieber pasingetosha hasa suala hilo la kumuwania Bieber, kwani Lulu pia ni mtu wa drama na kujiamini kwingi kama walivyo wawili hao toka Hollywood na pia wote watatu wapo rika moja.

No comments:

Post a Comment